Yanga, Azam vitani ligi kuu Tanzania Bara - LEKULE

Breaking

18 Feb 2015

Yanga, Azam vitani ligi kuu Tanzania Bara



Vita ya kugombea usukani wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya vilabu ya Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kati za Azam FC na Yanga inaendelea Alhamis.

Baada ya kushinda mechi zao za CAF nyumbani,Yanga ikiwafunga BDF XI ya Botswana (2-0)

katika kombe la Shirikisho na Azam ikiwafunga El-Merreikh ya Sudan (2-0)

katika kombe la Klabu Bingwa Afrika, timu hizo sasa zinaelekea nguvu katika mechi za

ligi, ikiwa pia ni kama sehemu ya maandalizi ya mechi zao za marudiano za

ugenini.

Yanga watasafiri hadi Botswana na Azam wataenda Khartou, Sudan wakitafuta

ushindi ili kusonga mbele baada ya Juma moja lijalo. Kuelekea mechi zao za Ligi Kuu Alhamis, kila timu

ina pointi 25,Azam ikiongoza kwa tofauti ya goli moja. Yanga itacheza na Tanzania Prisons mjini

Mbeya na Azam watacheza na Ruvu Shooting mkoa wa Pwani.

Kocha wa Yanga, Hans Pluijm ametamba kushinda, huku akikabiliwa na kibarua kigumu kingine dhidi ya Mbeya

City wikiendi hii mkoani Mbeya, kwa lengo la kuongoza ligi yenye ushindani mkubwa.

Akizungumza jana, msemaji wa Azam, Jafar Iddi amesema baada ya kuwafunga Mtibwa

Sugar 5-2 majuma mawili yaliyopita, sasa ni Azam ya Ruvu Shooting katika jitihada za kukaa mbali na Yanga katika msimamo

No comments: