HINA:NAKSHI NAKSHI INAYOPENDWA ZAIDI PWANI - LEKULE

Breaking

15 Jan 2015

HINA:NAKSHI NAKSHI INAYOPENDWA ZAIDI PWANI









Hina ( Heena )  ni  aina ya urembo ambao umekuwa ukitumiwa na watu wengi  hapa nchini Tanzania  hususani katika  maeneo ya pwani.

Kwa mujibu wa wataalamu wa Hina wanasema kuwa  zipo aina mbalimbali za michoro ya hina kila moja ikiwa na muonekano tofauti na nyingine.

Hata hivyo  mara nyingi aina hizi hutofautiana kulingana na mteja, mfano hina ya mtu anayetaka kufanya harusi ni tofauti kabisa  wasichana au akinamama wa nyumbani.

Nianzie  kuzungumzia aina ya Hina ya harusini,Hina hii huwa na maua makubwa na yaliyojaa tofauti na mingine. Si hivyo tu michoro hiyo huchukua sehemu kubwa ya maungo. Kwa mfano ikiwa ni mikononi, basi hupakwa hadi kwenye viwiko au kuanzia chini hadi juu kabisa

Katika hatua nyingine Hina kwa Wanaume hujulikana  kama tattoo.Wanaume hupenda kuchora juu kabisa ya mkono.

Hata hivyo kwa upande wa  watoto, hina hutumiwa na watoto hususan wa kike katika sikukuu hasa za Kiislamu kama vile Eid na  Maulid

No comments: