SHINAWATRA AJARIBU KUDHIBITI GHASIA. - LEKULE

Breaking

18 Dec 2013

SHINAWATRA AJARIBU KUDHIBITI GHASIA.

BANGKOK........,Waziri Mkuu wa Thailand,Yingluck Shinawatra ameanza kuitumia sheria maalumu ya usalama katika mji mkuu,Bangkok na katika sehemu za karibu ya mji huo baada ya waandamanaji kuzivamia wizara muhimu,kwa lengo la kuangusha serikali.Sheria hiyo maalumu ambayo imeshaanza kutumika katika wilaya kadhaa za mji mkuu,inawapa polisi mamlaka zaidi ya kuzifunga barabara,kutoa amri ya kuwazuia watu kutoka majumbani mwao na kupiga marufuku mikusanyiko ya watu.Maandamano makubwa tokea mwaka 2010 yanafanyika nchini Thailand kumpinga Shinawatra na nduguye Thaksin Shinawatra.

No comments: