HEKAHEKA Makosa ya Mochwari Tanga yaifikia #Hekaheka - LEKULE

Breaking

14 Mar 2016

HEKAHEKA Makosa ya Mochwari Tanga yaifikia #Hekaheka

March 14 2016 kupitia Hekaheka ya Clouds FMGeah Habib ametuletea Hekaheka iliyotokea Tanga hii  ni baada ya ndugu kuchanganya Maiti  katika Hospitali ya Bombo, Tanga, wakwanza kuchukua mwili wa marehemu walishamfanyia taratibu za mazishi na kuzika, ndipo badae walipo lazimika kufukua mwili baada ya kugundua siyo ndugu yao.
Maeneo ya Mikanjuni kulitoke msiba wa mzee aliyefahamika kwa jina la mzee Mhina ndipo walipompeleka kumuifadhi katika Hospitali ya Bombo, na kesho yake saa nne tulienda kuchukua maiti yetu kwa ajili ya kwenda kuzika tulifanikiwa kuzika lakini badae uongozi wa Bombo ulifika na kutuambia ile maiti sio yetu‘>>> Mkazi
Aliyeenda kuchukua mwili wa marehemu Hospitali ni Baba Mdogo, kuuosha pia alisismamia yeye baba mdogo na walivyorudi nyumbani baba mdogo alikata watoto wasione maiti ya baba yao mwisho wa siku ili bidi tufukue tuwape mwili wao na sisi tuchukue mwili wetu>>>Shuhuda

No comments: