Kesi Ya Hynes Kiwia ( Chadema ) Kupinga Matokeo Ya Ubunge Jimbo La Ilemela Jijini Mwanza Yafutwa - LEKULE

Breaking

11 Jan 2016

Kesi Ya Hynes Kiwia ( Chadema ) Kupinga Matokeo Ya Ubunge Jimbo La Ilemela Jijini Mwanza Yafutwa


Mahakama kuu kanda ya Mwanza leo imefuta rasmi kesi ya madai ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa mbunge jimbo la Ilemela.
 
Kesi hiyo imefutwa kutokana na ombi maalumu la mleta shitaka Hynes Kiwia kutaka kupunguziwa gharama za kuendesha keshi hiyo jambo ambalo lilishindikana kutokana na ombi hilo  kutokidhi vigezo

Katika shauri hilo lililofunguliwa mwaka jana Hyness Kiwia aliyekuwa mbunge wa jimbo la ilemela aliwashitaki Angelina Sylivester Mabula ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo hilo.


Shauri hilo limefutwa na msajili wa mahakama kuu kanda ya mwanza Eugenia gerald na kushuhudiwa na mawakili wa pande zote mbili

No comments: