Wanyarwanda Wengi Waunga Mkono Mabadiliko ya Katiba Kumruhusu Paul Kagame Kuendelea Kutawala - LEKULE

Breaking

19 Dec 2015

Wanyarwanda Wengi Waunga Mkono Mabadiliko ya Katiba Kumruhusu Paul Kagame Kuendelea Kutawala



Wanyarwanda wameunga mkono kwa wingi marekebisho ya katiba ambayo yatamruhusu Rais Paul Kagame kuendelea kuongoza, matokeo ya awali ya kura ya maoni yanaonyesha.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inasema 98% ya wapiga kura wameunga mkono marekebisho hayo ya katiba ambayo yatamruhusu Bw Kagame kuwania kwa muhula mwingine mwaka 2017, baada yake kumaliza muhula wa pili.
Tume hiyo imesema wilaya 21 kati ya wilaya 30 zimechapisha matokeo yake kufikia sasa.
Matokeo kamili yatatolewa baadaye leo Jumamosi.

No comments: