SHULE YA CATTON GROVE YA UINGEREZA YATOA MSAADA AMANI ORPHANAGE CENTRE, BAGAMOYO - LEKULE

Breaking

17 Nov 2015

SHULE YA CATTON GROVE YA UINGEREZA YATOA MSAADA AMANI ORPHANAGE CENTRE, BAGAMOYO

  Mratibu wa Wafanye Watabasamu ambaye pia ni mchora vibonzo nchini, Nathan Mpangala akimkabidhi sare za shule mmoja wa malaika kituoni hapo. Aliyetupia koti ni Mwakilishi wa TNTA nchini, Bw. Mussa Mussa Zaidi kuhusu Wafanye Watabasamu tembelea: https://www.facebook.com/wafanyewatabasamu
 Rafiki wa Wafanye Watabasamu, Mussa Sango akionesha upendo.
 Watoto wakizitathmini zawadi zao.
 Watoto wakionesha furaha yao.
 Mkurugenzi wa kituo cha Amani Orphanage Centre, Bi. Margareth Mwegalawa akiwa amempakata mtoto yatima anayelelewa kituoni hapo. Mtoto huyo alitupwa Chalinze miezi ya karibuni.
 Kutoka kulia, Nathan Mpangala (Mratibu Wafanye Watabasamu), Mussa Mussa (Mwakilishi TNTA), Amani Abeid (Rafiki wa Wafanye Watabasamu) na matroni wa kituo hiko wakiangalia tenki la maji kituoni hapo. Mnara wa tenki hili umetolewa na walimu wa Shule ya Msingi ya Catoon Grove.
 Mratibu wa Wafanye Watabasamu Nathan Mpangala na Mwakilishi wa TNTA Mussa Mussa walitafakari jinsi ya kuingia jikoni kituoni hapo.
Wafanye Watabasamu haikuwaacha hivi hivi, watoto wakapata nafasi ya kucheza na rangi. Pichani rafiki wa Wafanye Watabasamu, Amani Abeid akijiachia na malaika hao.

Watoto kituo cha yatima (Amani Orphanage Centre) kilicho katika Kijiji cha Zinga, Bagamoyo wakipokea ugeni wa marafiki wa Wafanye Watabasamu uliowatembelea jana. Marafiki wa Wafanye Watabasamu kwa kushirikiana na The Tanzania Norwich Association (TNTA) walikwenda kituoni hapo kukabidhi sare za shule pea 32, mabegi ya shule 32, mikebe na madaftari vilivyotolewa na walimu wa Shule ya Msingi ya Catton Grove ya Uingereza. (Picha zote na Wafanye Watabasamu).

No comments: