Mkurugenzi Mpya wa Hospitali ya Muhimbili Aliyeteuliwa na Rais Magufuli Aanza Kazi Rasmi Baada ya Mkurugenzi Wa Zamani Kufutwa Kazi - LEKULE

Breaking

11 Nov 2015

Mkurugenzi Mpya wa Hospitali ya Muhimbili Aliyeteuliwa na Rais Magufuli Aanza Kazi Rasmi Baada ya Mkurugenzi Wa Zamani Kufutwa Kazi


Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dk Hussein Kidanto (kushoto) akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru (kulia) ambaye ameteuliwa juzi na Rais John Pombe Magufuli. Juzi Rais Magufuli amemuamishia Dk Kidanto katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru ambaye ameteuliwa juzi na Rais John Pombe Magufuli akizungumza na menejimenti ya hospitali hiyo jana.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma (MNH), Aminiel Aligaesha (kushoto) na mwanasheria wa hospitali hiyo, Veronica wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.
Baadhi ya wakurugenzi wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma (MNH), Aminiel Aligaesha (kulia) na akimtambulisha Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali hiyo Profesa Lawrence Mseru kwa kamati tendaji, wakurugenzi, wakuu wa idara, mameneja wa majengo ya Kibasila, Sewahaji, Mwaisela na Jengo la Watoto.
Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru (kulia) akizungumza na kamati tendaji, wakurugenzi, wakuu wa idara, mameneja wa majengo ya Kibasila, Sewahaji, Mwaisela na Jengo la Watoto.

Kamati Tendaji, wakurugenzi, wakuu wa idara, mameneja wa majengo ya Kibasila, Sewahaji, Mwaisela na Jengo la Watoto wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi mpya wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru  

No comments: