Dr Yash Gulati,
Senior Spine and Joint Replacement Surgeon
at Apollo Hospitals; Delhi
|
Na Mwandishi Wetu,
Maendeleo
katika njia za ufanyaji kazi pamoja na matumizi ya teknolojia
yanavyokuwa kwa kasi yanaweza kutufanya tuamini tumepunguza maumivu
katika viungo vyetu vya mwili ila si hivyo. Tunatumia magari, mitandao
mbalimbali ambayo vizazi vilivyopita havijawahi kuota kutumia.
Mabadiliko haya mapya katika maisha yetu yenye msisitizo mdogo katika
uimarishaji wa viungo umechukua hatamu na kuathiri maisha yetu kwa maana
mwili wa binadamu ni ule ule toka miaka milioni iliyopita. Na hiyo
inasababisha kuongeza matukio mengi ya maumivu ya mgongo kwa sababu uti
wa mgongo umekwisha athirika.
Watu
wengi lazima wakutwe na maumivu ya uti wa mgongo walau mara moja katika
vipindi vya maisha yao. Sehemu kubwa inayoathirika katika uti wa mgongo
ni sehemu ya chini kabisa na sehemu ya shingoni kwa sababu sehemu hizo
ndizo zina beba uzito mkubwa wa mwili kila siku. Sababu nyingine
zinazosababisha maumivu ya mgongo ni kuharibika kwa diski, mgandamizo
katika vertebra na kudhoofika kwa mifupa kutokana na upungufu wa tishu
(osteoporosis) kutokana na umri inaweza kusababisha mgandamizo wa
vertebra na kusababisha ufa.
Zipo
zaidi ya sababu 100 zinazoweza kusababisha maumivu ya mgongo upande wa
chini; matukio ambayo yanaweza kusababisha maumivu mgongoni na
yasitambulike. Sababu maalumu ya kuleta maumivu ya mgongo inabaki kuwa
ni kuharibika au kuvunjika kwa sehemu zinazounga uti wa mgongo kutokana
na pozi baya la ukaaji.
Watafiti
wameonyesha kuwa ukaaji mbovu katika viti au sehemu yoyote na kutofanya
kazi inayoshughulisha misuli ya mgongo kunachangia maumivu ya mgongo na
hata udhaifu katika uti wa mgongo. Maumivu katika mgongo na shingoni ni
moja ya sababu za msingi za wafanyakazi kuchukua likizo maofisini.
Asilimia 50 ya wafanyakazi wanajikuta wakipata maumivu ya mgongo na
shingo mara moja kwa mwaka.
Kwa
mujibu wa Dk. Yash Gulati, Mpasuaji Mwandamizi wa uti wa mgongo na
viungo kutoka hospitali za Apollo; Delhi, habari njema ni kwamba
asilimia 75 ya matatizo yote yanayohusisha maumivu ya mgongo
yanaepukika, na asilimia iliyobaki yana epukika, mengine yanatibika na
mgonjwa kurudi katika hali yake ya awali ndani ya muda mfupi.
Baadhi
ya sababu za kwa nini kumekuwa na ongezeko la matukio ya maumivu ya uti
wa mgongo ni kutokana na mabadiliko ya maisha kwa watu wanaoishi
mijini. Wengi huwa wanaanza siku zao kwa kupoteza muda mwingi kwenye
magari.
Kuendesha
gari kwa muda mrefu kunapelekea maumivu katika sehemu ya chini ya
mgongo. Kuepuka hilo, siti ya dereva inatakiwa iwekwe vizuri. Kama kuna
uwazi kati ya siti na mgongo wa dereva, uwazi huo uondolewe aidha kwa
kuweka mto au kusogeza kiegemeo cha kiti mbele. Magoti yanatakiwa yawe
juu kidogo. Hiyo inaweza kuwa hivyo iwapo utajaribu kusogeza kiti mbele
au nyuma. Kama upo uhitaji wa kuendesha gari muda mrefu kama sehemu ya
kazi, ni vyema kuendesha kupata mapumziko mafupi ya kushuka na
kujinyoosha na kisha kuendelea na safari. Wakati wa kushuka ni vyema
mguu uanze kufika chini na sio kuruka.
Sababu
kubwa ya pili iliyogundulika katika kuleta maumivu mgongoni ni hizi
kazi za kukaa kwenye kiti muda mrefu (white-collar job) ambazo
wafanyakazi wanapoteza muda mwingi mbele ya kompyuta, hawakai katika
viti vile ipasavyo au wakati ofisi ina samani zinazoathiri ukaaji wa
wafanyakazi. Ni vyema kila mfanyakazi ahakikishe kiti chake kipo katika
kimo kinachoendana na meza yake ili kutoumiza mgongo. Kompyuta ziwe
katika umbali unaofaa ili kuepuka mtu kukunja mgongo ili aweze kusoma au
kuandika chochote katika kompyuta.
Uzito
uliozidi kutokana na kutofanya mazoezi kunaweza kupelekea maumivu ya
mgongo pia. Kwa mujibu wa Dk. Yash Gulati, uzito uliozidi unapoleta
kitambi mara nyingi hupelekea kujikunja kwa mgongo na kuanza kuleta
maumivu katika viungo na maungio katika mgongo. Ni muhimu sana kwa kila
mtu kuhakikisha ana uzito sawia na urefu wake, ili kupunguza madhara ya
kuathiri uti wa mgongo.
Sababu
nyingine inayotokea mara kwa mara ya maumivu ya mgongo ni kusogea au
kuharibika kwa diski alisema Dk. Yash Gulati wa Hospitali za
Apollo;Delhi. Hii inatokea pale ganda la nje la diski lililo kama
shokomzoba katikati ya mifupa miwili ya vertebral,linapochanika na
kusababisha uvujaji wa ute mwepesi uliopo ndani.
Kulingana
na sehemu diski ilipo, inaweza kubana neva za uti wa mgongo na
kupelekea maumivu makali na kupooza kwa miguu na mikono. “asilimia
tisini ya wenye tatizo la diski kuharibika wanapewa huduma kwa njia
maalumu ya mazoezi ya viungo (physiotherapy) na mapumziko ya kutosha. Ni
mmoja kati ya kumi watakao hitaji upasuaji mdogo (discectomy) wa kuitoa
ile diski iliyosogea na kubana neva” alisema Dk. Gulati.
Apollo
ni moja ya hospitali chache zilizofikia kiwango cha juu cha ubora wa
matibabu na kufurahia matunda ya katika eneo adimu la upasuaji katika
uti wa mgongo. Upasuaji wa kuondoa diski unafanyika kwa kuchukua
tahadhari kubwa ya kupunguza madhara ambayo mgonjwa anapona mapema bila
uvimbe mkubwa na pia kuweza kuendelea na kazi zake za kawaida.
Imetolewa na:
Dk. Yash Gulati, Mpasuaji Mwandamizi wa uti wa mgongo na viungo kutoka hospitali za Apollo; Delhi.
No comments:
Post a Comment