Ujambazi Dar, 63 wamekamatwa na silaha zao ndani ya siku 7 - LEKULE

Breaking

10 Apr 2016

Ujambazi Dar, 63 wamekamatwa na silaha zao ndani ya siku 7



 leo April 8 2016 Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam kupitia kwa Kamishna Simon Sirro, limetangaza kuwakamata majambazi  63 wa matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha katika oparesheni iliyofanyika ndani ya wiki moja.
Kamanda sirro amesema ‘Tarehe 07/04/2016 majira ya saa 09:15 usiku katika eneo la Vingunguti uwanja wa Koroni, Kikosi maalum cha kupambana na majambazi kilifanikiwa kukamata silaha aina ya SMG iliyokatwa kitako katika bonde la mto msimbazi
katika tukio lingine, tarehe 4/4/2016 majira ya saa 08:45 asubuhi katika barabara ya Ally Bin Said, Askari wakiwa kwenye operesheni ya kusaka wahalifu wa makosa mbalimbali katika wilaya ya Kinondoni, walifanikiwa kukamata silaha mbili Rifle ambazo hazikuwa na risasiSimon Sirro
Baada ya kuyataja matukio yote  yaliyopelekea kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa ujambazi, kamanda Sirro pia hakuacha kuliongea hili la kesho katika mechi ya Yanga dhidi ya Al-Alhly ya Misri 
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi tumejipanga ipasavyo kuhakikisha mechi hiyo inachezwa katika hali ya usalama, na natoa tahadhari kuwa hairuhusiwi kwa shabiki yoyote kuingia uwanjani akiwa na vifaa vya hatari kama Mapanga N.kSimon Sirro

No comments: