MATUKIO 10 YALIYOWATOA MACHOZI WACHEZA SOKA ULAYA - LEKULE

Breaking

27 Mar 2016

MATUKIO 10 YALIYOWATOA MACHOZI WACHEZA SOKA ULAYA

cover19
Mpira wa miguu ni mchezo wa aina yake na ndiyo mchezo pendwa kuliko yote duniani. Baada ya mchezo wa kwa kawaida kuna matokeo ya aina tatu kushinda, kufungwa na kutoka sare.
Watu wanatofautiana hisiakatika kupokea matokeo, tumekuwa tukishuhudia hisia tofauti kutoka kwa mashabiki, wachezaji au makocha baada ya timu zao kushinda au kupoteza michezo yao.
www.shaffihdauda.co.tz inakuletea top 10 ya matukio yaliyowafanya wachezaji wamwage machozi uwanjani.
10. Mario Balotelli– fainali ya Euro 2012
Balo
Mchezaji wa kimataifa wa Italia Mario Balotelli alilia kwenye mchezo wa fainali za Euro mwaka 2012 baada ya timu yake kupoteza mchezo kwa bao 4-0 dhidi ya Hispania.
Alijikuta akiangua kilio pale aliposhuhudia nahodha wa Hispania Iker Casillas akinyanyua ndoo.
Jack Wilshere –Arsenal v Birmingham, fainali ya Carling Cup
Wilshere 2
Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere alijikuta akimwaga machozi pale Arsenal iliporuhusu bao dakika ya 89 dhidi ya Birmingham City kwenye mchezo wa fainali ya Carling Cup baada ya kutokea mkanganyiko kati ya Wojciech Szczesny na Laurent Koscielny.
Goli hilo likazima kabisa ndoto za Arsenal kumaliza ukame wa aji kwenye kikosi chao.
Wachezaji pamoja na kocha wao walichanganyikiwa na kichapo hicho cha dakika za lala salama. Ilikuwa ni miaka sita imepita tangu timu yao ichukue kombe kwa mara ya mwisho na hiyo ilikuwa ngumu kukubali matokeo hayo kwenye mchezo wa fainali.
8. Cristiano Ronaldo– fainali ya Euro 2004
Ronaldo crying
Ni miaka 12 sasa tangu Cristiano Ronaldo aibuke kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ureno. alikuwa na miaka 19 wakati Ugiriki wanaikandamiza Ureno kwa bao 1-0 kwenye fainali ya michuano ya Euro iliyofanyika kwenye ardhi ya kwao  mwaka 2012. Baada ya filimbi ya mwisho, Ronaldo alikaa chini na kuanza kumwaga machozi.
7. Ronaldinho–Atletico Mineiro
Dinho
Ronaldinho alianza kulia baada ya kutupia kambani. Muda huohuo akapiga magoti na kuanza kulia huku wachezaji wenzake wawakiwa wamemzunguka.
Lilikuwa ni tukuio la kushangaza, hasa kutoka kwa mchezaji maarufu wa aina yake ambaye hutabasamu muda wote akiwa uwanjani.
Kilio hicho kilitokana na majonzi aliyokuwa nayo Ronadinho kutokana na kufiwa na baba yake wa kambo aliyefariki siku chache kabla ya mchezo kutoka na shambulio la moyo (heart attack)
6. John Terry–Champions League nusu fainali
Terry
Baada ya kichapo cha bao 3-1 dhidi ya Atletico Madrid kwenye michuano ya UEFA msimu wa 2013/24 hatua ya nusu fainali, nahodha wa Chelsea John Terry alishindwa kuelewa ni kwa jinsi gani timu yake imetupwa nje ya mashindano. Alishindwa kujizuia na kuanza kumwaga machozi.
5. Andrea Pirlo–Euro 2012 Final
Pirlo
Licha ya kuwa mchezaji aliyebarikiwa kiwango bora kwenye kikzazi chake na kufanikiwa kutwaa karibu mataji yote muhimu, lakini kabati lake halina taji la mataifa ya Ulaya (European Championships).
Mwaka 2012 alikaribia kutwaa kombe hilo na kuongeza la yale ya ligi ya Italia (Scudetto), Champions League na kombe la dunia.
Wakati wa michuano hiyo ambayo alitajwa kuwa man of the match kwenye michezo mitatu huku timu yake ikifuzu hatua ya fainali lakini tukio kubwa la kukumbukwa kwenye mashindano hayo ni ile penati aliyofunga dhidi ya England katika changamoto za mikwaju ya penati.
Kwa bahati mbaya alishindwa kuisaidia timu yake ya taifa kutwaa taji dhidi ya Hispania kwa kupoteza kwa bao 4-0 kwenye mchezo wa fainali.
Fundi huyo wa mpira alijikuta akifuta machozi kwa viganja vyake vya mikono licha ya kufanya mambo makubwa kwenye fainali hizo.
4. Luis Suarez–Liverpool v Crystal Palace, Premier League (2013/14)
Suarez
Baada ya Crystal Place kupiga bao 3 ndani ya dakika 10 wakitoka nyuma kwa bao 3-0 hadi sare ya magoli 3-3 dhidi ya Liverpool, nyota wa ‘Majooo wa Jiji’ wakati huo Luis Suarez alijifunika uso kwa jezi yake huku akilia.
Sare hiyo ilikuwa inafuta ndoto za Liverpool kushinda jombe la ligi ya EPL kwa msimu huo. Msimu wa 2023-2014 ulikuwa ni msimu ambao Liverpool walikaribia sana kushinda taji hilo kuliko wakati wowote.
“Ilikuwa inaumiza kukosa kombe la ligi. Huwezi kufungwa magoli matatu ndani ya dakika 10. Sikuwahi kuduwazwa uwanjani kwa kiasi kile”, alisema Suarez baada ya mchezo.
3.David Luiz – Brazil 2014, nusu fainali kombe la dunia
David Luis
Akikongoza kikosi cha Brazil kama nahodha kwenye mchezo wa kombe la dunia lakini alikiongoza kuyaaga mashindano hayo. Kukiongoza kikosi cha Brazil ni ufahari lakini haikuwa hivyo kwa David Luis.
Mchezo ulimalizika huku Brazil ikibebeshwa zigo la magoli 7-1 na Ujerumani na ikawa aibu kwake kuingoza nchi yake, alijikuta akibubujikwa na machozi mbele ya mashabiki waliofurika uwanjani kuishangilia timu yao wakiamini itafanya vizuri mbele ya wajerumani.
2. Iker Casillas– fainali ya Champions League 2014
CASILLAS
Iker Casillas alishibwa kuzuia furaha yake wakati walipokaribia kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa Ulaya kwa mara ya 10 dhidi ya Atletico Madrid kwenye mchezo wa fainali uliopigwa Lisbon.
Atletico waliibana Madrid na kujikuta ikishindwa kupata bao la kusawazisha hadi dakika ya 92 baada ya Atletico kuwa mbele kwa bao 1-0. Sergio Ramos aliisawazishia Madrid dakika ya 93 na kuufanya mchezo huo kuongezewa dakika (extra time)
Mwisho wa siku Real Madrid ikashinda mchezo huo kwa bao 4-1 na kusherekea taji la 10 la Ulaya.
1.David Beckham – mechi yake yake ya mwisho PSG
Bechkam
Dakika ya 82 akiwa anafanyiwa mabadiliko kwenye mchezo wake wa mwisho akiwa mchezaji wa Paris Saint Germain, David Beckham aliangua kilio uwanjani.
Mashabiki 45,000 wakisimama kwa heshima kwa ajili ya nyota huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England, aliwakumbatia wachezaji wenzake pamoja na wake wa timu pinzani kabla ya kutoka kumpisha Ezequiel Lavezzi.
Baada ya mechi wachezaji wenzake walimchukua na kumrusha hewani kwa heshima.

No comments: