Malawi yatekeza tani 2 za pembe kutoka TZ - LEKULE

Breaking

14 Mar 2016

Malawi yatekeza tani 2 za pembe kutoka TZ



Malawi imeteketeza tani 2.6 ya pembe za ndovu ambazo zilinaswa na maafisa wa usalama zikitokea nchi jirani ya Tanzania.

Meno hiyo 781 ya tembo ambayo inakisiwa kugharimu takriban dola milioni tatu ilipatikana baada ya operesheni dhidi ya ulanguzi na uwidaji haramu.

Mkurugenzi wa idara inayosimamia mbuga za wanyama pori Bright Kumchedwa, amesema kuwa hiyo ni ishara ya kwanza na dhabiti kutoka kwa Malawi kuwa haitaruhusu tena ardhi yake kutumika kulangua bidhaa za uwindaji haramu.

Hafla ya hiyo ya kihistoria ilifanyika katika eneo la Mzuzu kaskazini mwa nchi hiyo.
Kenya inatarajiwa kutekeleza hatua kama hiyo mwishoni mwa mwezi huu.
Kenya imekamata takriban tani 120 ya meno ya ndovu.

No comments: