Toka Bungeni : Bunge Latengua Kanuni Ya 94 (1) - LEKULE

Breaking

1 Feb 2016

Toka Bungeni : Bunge Latengua Kanuni Ya 94 (1)

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetengua kanuni ya 94 (1) ya kanuni za kudumu za bunge za mwaka 2006 ili kuliwezesha bunge  kujadili mpango wa serikali utakaotaumika kwa muda wa mwaka wa fedha 2016 & 2017.

Akitengua kanuni hiyo, Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu katika Serikali ya Awamu ya Tano, Jenista Mhagama amesema kwamba bunge lilitakiwa likae kama kamati mwezi Nonemba ili liweze kujadili mpango wa serikali lakini kutokana na uchaguzi mkuu uliokuwepo nchini kazi hiyo ilishindikana.

Kwa msingi huo kutokana na uwezo wa bunge kupitia ibara ya 63 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowezesha bunge kujadili mipango ya serikali,kwa muda muafaka serikali imeamua kutengua kanuni ili bunge likae kama kamati kwa muda wa siku 5 ili kujadili mpango wa serikali ili wabunge waweze kuishauri serikali kabla ya bunge la bajeti.


Aidha mpango huo ulishindwa kujadiliwa bungeni Ijumaa iliyopita kutokana na kanuni za bunge kukiukwa kwa kusomwa bila kutengua kanuni ya 94(1).

No comments: