Watu 62 wanamiliki nusu ya utajiri wa dunia - LEKULE

Breaking

19 Jan 2016

Watu 62 wanamiliki nusu ya utajiri wa dunia

Davos Weltwirtschaftsforum 2016
Matajiri zaidi 62 duniani, hivi sasa wanamiliki zaidi ya nusu ya utajiri wa wakaazi wote wa dunia, limesema shirika la hisani la Oxfam, kuelekea mkutano wa kiuchumi wa dunia - World Economi Forum (WEF) Davos, Uswis.
Ripoti hiyo ya Oxfam inasema utajiri wa watu hao 62 matajiri zaidi umeongezeka kwa asilimia 44 tangu mwaka 2010, huku utajiri wa watu maskini zaidi bilioni 3.5 umeshuka kwa asilimia 41. Ripoti hiyo iliyopewa kichwa cha habari kisemacho: "Uchumi wa asilimia 1", inabainisha kuwa wanawake wanaathirika zaidi na ukosefu wa usawa duniani.
Karibu nusu ya matajiri zaidi wa dunia wanatokea nchini Marekani, 17 barani Ulaya na waliosalia wanatoka katika mataifa yakiwemo China, Brazil, Mexico, Japan na Saudi Arabia.
Moja ya mambo muhimu yaliyoainishwa katika ripoti ya Oxfam ambayo yanayochangia ukosefu wa usawa duniani ni kupungua kwa mgao wa pato la taifa linalokwenda kwa wafanyakazi karibu katika mataifa yote yalioendelea na yanayoendelea, na kuongeza kuwa wengi wa wafanyakazi wanaolipwa kiasi kidogo zaidi cha mshahara ni wanawake.

Pengo la walio na wasio nacho lazidi kupanuka.

No comments: