Matajiri
zaidi 62 duniani, hivi sasa wanamiliki zaidi ya nusu ya utajiri wa
wakaazi wote wa dunia, limesema shirika la hisani la Oxfam, kuelekea
mkutano wa kiuchumi wa dunia - World Economi Forum (WEF) Davos, Uswis.
Ripoti
hiyo ya Oxfam inasema utajiri wa watu hao 62 matajiri zaidi umeongezeka
kwa asilimia 44 tangu mwaka 2010, huku utajiri wa watu maskini zaidi
bilioni 3.5 umeshuka kwa asilimia 41. Ripoti hiyo iliyopewa kichwa cha
habari kisemacho: "Uchumi wa asilimia 1", inabainisha kuwa wanawake
wanaathirika zaidi na ukosefu wa usawa duniani.
Karibu
nusu ya matajiri zaidi wa dunia wanatokea nchini Marekani, 17 barani
Ulaya na waliosalia wanatoka katika mataifa yakiwemo China, Brazil,
Mexico, Japan na Saudi Arabia.
Moja ya
mambo muhimu yaliyoainishwa katika ripoti ya Oxfam ambayo yanayochangia
ukosefu wa usawa duniani ni kupungua kwa mgao wa pato la taifa
linalokwenda kwa wafanyakazi karibu katika mataifa yote yalioendelea na
yanayoendelea, na kuongeza kuwa wengi wa wafanyakazi wanaolipwa kiasi
kidogo zaidi cha mshahara ni wanawake.
Pengo la walio na wasio nacho lazidi kupanuka.
No comments:
Post a Comment