WANAFUNZI 538 WATUNUKIWA VYETI VYAO KATIKA MAHAFARI YA NANE YA CHUO CHA TRA LEO JIJINI DAR ES SALAAM. - LEKULE

Breaking

16 Jan 2016

WANAFUNZI 538 WATUNUKIWA VYETI VYAO KATIKA MAHAFARI YA NANE YA CHUO CHA TRA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

WANAFUNZI 538 wa chuo cha Mamlaka ya Mapato (TRA) wametunukiwa vyeti vyao leo katika mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.

Pia wahitimu hao wameaswa kuwa waadilifu katika kazi zao kwani taaluma yao ni ukusanyaji wa mapato ya sehemu zao za kazi.

Wameaswa hayo na  Naibu waziri wa Fedha na Mipamgo, Ashatu Kijaji wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa mahafali ya nane ya chuo cha Mamlaka ya Mapato (TRA) yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.

amesema kuwa wahitimu wa chuo hicho wafanye kazi kwa weredi na uaminifu  kwani wasipofanya hiyo hawataweza kufanya kazi hayo vile inavyopaswa.

Chuo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kitajengwa kingine huko  kibaha mkoani pwani ili kuongeza wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri kwani chuo kilichopo Mwenge kimezungukwa na viwanda.




 Naibu waziri wa Fedha na Mipamgo, Ashatu Kijaji akizumgumza na wahitimu wa chuo cha Mamlaka ya mapato Tanzania TRA leo katika mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar es Salaam



 Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiwa katika mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Makamu Mkuu wa Chuo, Lewis Ishemoi akiwaita majina wanafunzi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) leo katika mahafali ya nane ya chuo hicho ikiwa wahitimu 538 wamehitimu mafunzo yao katika chuo hicho jijini Dar es Salaam leo.Wanafunzi wakivaa kofia zao mara baada ya kutunukiwa katika mahafali yaliyofanika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.


 Naibu waziri wa Fedha na Mipamgo, Ashatu Kijaji akiwatunukia vyeti wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo yao katika mahafali yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.


 Wahadhiri wakiwitunukiwa vyeti pamoja na zawadi mbalimbali katika mahafali ya nane ya chuo cha mamlaka ya mapato (TRA) leo jijini Dar es Salaam. kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Alphayo Kidata na Makamu Mkuu wa Chuo, Lewis Ishemoi.


Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

No comments: