WAHITIMU 67 WA MAFUNZO YASIYO RASMI WA CHUO CHA VETA WAPATA VYETI LEO JIJINI DAR ESALAAM. - LEKULE

Breaking

15 Jan 2016

WAHITIMU 67 WA MAFUNZO YASIYO RASMI WA CHUO CHA VETA WAPATA VYETI LEO JIJINI DAR ESALAAM.

WAHITIMU 67 wasio katika Mfumo Rasmi watunukiwa vyeti katika kuwarasimisha katika ujuzi waliopata  katika maeneo yao ya kazi.

Akizungumza katika mahafali hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA),Geofrey Sabuni amesema kuwa wataendelea kutoa mafunzo hayo ili kuwatambua mafundi wa mitaani ambao wamekuwa hatambuliki kutokana na kukosa mafanzo katika taasisi zinazotambulika.

Amesema kuwa nia ya kuwafikia watu 5000 katika kurasimisha kazi wanazozifanya kutokana na mchango mkubwa wa taifa huku wakiwa hawatambuliki.

Sabuni amesema kuwa VETA itahakikisha inaendelea kutoa mafunzo kwa vijana katika ujuzi mbalimbali pamoja na wale ambao hawako katika mfumo rasmi kuwatambua.

Aidha amesema kuwa katika jitihada zote kuna changamoto hivyo kwa wahitimu lazima waendelee kuongeza ujunzi wa mafunzo ya muda mrefu  katika kuwa wabobezi huku wakiwa na vyeti vinavyoonyesha ujuzi.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Veta Dar es Salaam,Violet Fumbo amesema katika mafunzo wanayotoa wanatambulika sehemu zote kutokana na mafunzo hayo kuingizwa katika mitaala.

Violet amesema katika mambo wanayoyafanya ni kutaka vijana kujituma katika ujuzi waliofanya kazi hiyo 



 Afisa mitihani wa chuo cha ufundi cha VETA kilichopo Temeke,Elishawake Lema akifungua sherehe za Mhafari kwa wanafunzi waliojiunga kozi ya muda mfupi ambayo Veta wameshirikiana na na shilika la kazi Duniani (ILO) kwa kutoa mafunzo hayo. mafunzo hayo ni Upishi, ufundi uwashi, ufundi wa magari na upambaji.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha ufundi stadi cha Veta, Geofrey Sabuni akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya muda mfupi katika chuo hicho leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkuu wa  Chuo cha ufundi stadi cha Veta, Violet Fumbo kulia akisoma lisala  mbele ya wahhitimu na mgeni rasmi katika mahafari ya muda mfupi ya chuo cha ufundi cha Veta leo jijini Dar es Salaam. waliokaa kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya mafunzo ya ufundi stadi (VETA), Geofrey Sabuni  Mwakilishi wa Shirika la Kazi (ILO), Albert Okal na Afisa mitihani wa chuo cha ufundi cha VETA kilichopo Temeke,Elishawake Lema.


Mwakilishi wa Shirika la Kazi (ILO), Albert Okal akizungumza na wahitimu wa chuo cha mafunzo stadi ya ufundi cha Veta jinsi walivyo shirikiana na chuo hicho ili kuondoa okosefu wa ajira kwa baadhi ya vijana walioweza kufanikiwa kujiunga na kozi ya muda mfupi katika chuo hicho.
Walimu waliofanikisha mafunzo kwa wanafunzi na wahitimu wa leo katika chuo hicho.



Wahitimu wakisimsikiliza mgeni rasm katika mahafari hayo leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wakiongalia matisheti yao yakiwa na nembo ya shirika la kazi duniani (ILO) leo katika mahafari ya mafunzo hayo.


Katika mahafali hayo wametunukiwa vyeti vya kufuzu masomo yao katika chuo cha mafunzo ya ufundi Stadi (VETA) leo jijini Dar es Salaam.

Viongozi wa chuo wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wahitimu leo jijini Dar es Salaam.

No comments: