Uteuzi anaofanya Rais Magufuli umemfikia mpaka mstaafu JK leo. - LEKULE

Breaking

21 Jan 2016

Uteuzi anaofanya Rais Magufuli umemfikia mpaka mstaafu JK leo.

Alhamisi January 21 2016 ni siku nyingine ambayo Rais Magufuli kaendelea na moja ya majukumu yake kama Rais wa nchi, jukumu la leo ni kwamba kaendelea na uteuzi wa viongozi kwenye nafasi mbalimbali, uteuzi wa leo imelirudisha pia jina la Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mzee Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Magufuli amemteua Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam UDSM.
JPM VS JK
Rais Mstaafu JK ameteuliwa kushika nafasi hiyo ambayo ilikuwa wazi baada ya kufariki kwa Balozi Fulgence Kazaura aliyefariki February 2015.

No comments: