TIGO yafungua duka la kisasa Same - LEKULE

Breaking

18 Jan 2016

TIGO yafungua duka la kisasa Same


Katibu wa wilaya ya Same Mhe. Evagry Keiya (katikati) akikata utepe kufungua duka la Tigo Same, wanaoshuhudia ni Meneja wa huduma kwa wateja Tigo, Mwangaza Matotola(kushoto) na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata(kulia) mapema mwishoni wa wiki iliyopita.

Baadhi ya wafanyakazi wa Tigo  wakiwa katika tafrija ya ufunguzi wa duka la Tigo Same mapema wa mwishoni  wa wiki iliyopita.

Mkurungezi wa Tigo kanda ya kaskazini Bw.George Lugata akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa duka la Tigo Same mapema mwishoni wa wiki iliyopita.

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye tafrija ya kufungua duka la Tigo same wakisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Mh Evagry Keiya  mapema mwishoni wa wiki iliyopita.
Kampuni ya simu ya Tigo imefungua duka jipya la  same ambalo limepunguza adha kwa wateja wa kampuni hii ambao walikuwa wanatafuta huduma kwa wateja umbali mrefu toka kwa makazi yao 
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo Mkurungezi wa Tigo Kanda ya kaskazini Bw.George Lugata alisema uzinduzi wa duka hili ni moja ya mipango ya kampuni ya Tigo kusogeza huduma karibu na wateja wake.
“Kampuni ya tigo imeangalia fursa zilizopo katika eneo la Same ambapo kwa pamoja tumeiona ni jinsi gani tunaweza kusaidiana na wakulima na wafanya biashara kuweza kufanya huduma mabalimbali za kibenki kwa kutumia simu za mkononi”Alisema Lugata
Aliongeza kuwa ufunguzi huo unaendana na kuboresha muonekano wa duka hili kuwa wa kisasa
Lugata alisema kuwa duka hilo linalopatikana katika mtaa wa shule linategemea kuhudumia wateja wapatao mia tatu kwa siku wakipata huduma mbalimbali ikiwemo huduma za kuunganishwa kwenye intaneti, usajili wa laini za simu na kurudisha laini zilizopotea pia kununua simu za kisasa.

Kwa upande wa Katibu wa Mkuu wa Wilaya ya Same  Mhe. Evagry Keiya alipongeza hatua za Tigo za ufunguzi wa duka hili kwa kuwa utarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja wa wilaya ya sam

No comments: