RONALDO AVUNJA BANK ILI KUFUTA MACHUNGU YA KUKOSA BALLON D’OR - LEKULE

Breaking

13 Jan 2016

RONALDO AVUNJA BANK ILI KUFUTA MACHUNGU YA KUKOSA BALLON D’OR

Ronaldo akionesha mkoko wake mpya wa bei chafu aina ya Porsche Turbo S
Ronaldo akionesha mkoko wake mpya wa bei chafu aina ya Porsche Turbo S
Mara baada ya kukosa tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Ballon d’Or) iliyochukuliwa na mpinzani wake wa muda mrefu Lionel Messi, mshambuliaji wa Real Madrid na nahodha wa Ureno alionekana katika morali ya juu kabisa mara baada ya kupost picha katika mtandao wake wa Instagram akiwa ameketi na gari mpya aina ya Porsche Turbo S yenye thamani ya dola 146,000 za Marekani.
Ronaldo mwenye miaka 30 hivi sasa, alikosa tuzo hiyo ambayo ingekua ni ya nne kwake kama angetwaa laikini aliishuhudia ikienda kwa Lionel Messi wa Barcelona na kumfanya muargentina huyo kufikisha tuzo 5 tangu alipochukua 2009, 2010, 2011, 2012 na 2015.
Ronaldo amekosa tuzo ya Ballorn d'Or ambayo ilinyakuliwa na Messi endapo Ronaldo angetwaa tuzo hiyo, ingekuwa ni mara yake ya nne kuichukukua
Ronaldo amekosa tuzo ya Ballorn d’Or ambayo ilinyakuliwa na Messi endapo Ronaldo angetwaa tuzo hiyo, ingekuwa ni mara yake ya nne kuichukukua
Pamoja na Ronaldo kutokuchukua tuzo hiyo lakini ndiye aliyekua mfungaji bora wa mabao katika michuano yote msimu uliopita ingawa hakufanikiwa kuisaidia Real Madrid kutwaa taji lolote wakati Messi aliisaidia Barcelona kushinda mataji yote waliyoshiriki.
Lionel Messi akiwa na tuzo yake ya Ballon d'Or ya tano alitwaa siku chache zilizopita kwa kuwashinda Cristiano Ronaldo na Neymar
Lionel Messi akiwa na tuzo yake ya Ballon d’Or ya tano alitwaa siku chache zilizopita kwa kuwashinda Cristiano Ronaldo na Neymar
Akiongea na mtandao wa klabu yake ya Madrid, Cristiano amesema kuwa, siku zote hawezi kuacha kufurahisha mashabiki wake na wote wanaomsapoti huku akisisitiza kuwa atazidi kujituma kuisaidia Madrid kutwaa mataji, kufunga magoli mengi kila msimu, sanjari na kuwa sehemu ya timu (team player).
Sergio Ramos, Marcelo, Luka Modric na Ronaldo katika pose na uzo zao kikosi bora cha mwaka cha FIFA (FIFPro XI awards)
Sergio Ramos, Marcelo, Luka Modric na Ronaldo katika pose na uzo zao kikosi bora cha mwaka cha FIFA (FIFPro XI awards)

Ronaldo ambaye ndiye kinara wa mabao katika historia ya klabu ya Real Madrid hivi sasa mara baada ya kuvunja rekodi iliyokua inashikiriwa na legendari Raul Gonzalez, amesema ataendelea kufunga magoli na kuweka rekodi mpya ikiwemo kufikisha hata magoli 1000.

No comments: