Laurent Gbagbo akana mashtaka ICC - LEKULE

Breaking

29 Jan 2016

Laurent Gbagbo akana mashtaka ICC

Elfenbeinküste Präsident Laurent Gbagbo
Rais wa zamani wa Cote d'Ivoire Laurent Gbagbo amekana kuwa na hatia katika mashataka manne ya uhalifu dhidi ya ubinaadamu katika mahakama ya ICC, miaka mitano baada ya nchi yake kukumbwa na vurugu za uchaguzi.
Gbagbo pamoja na aliyekuwa waziri wake wa vijana Charles Ble Goude wote wawili wameyakanusha mashtaka yanayowakabili kuhusiana na kuhusika kwao katika machafuko yaliyotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 ambayo yalisababisha vifo vya watu 3,000 nchini humo. Charles Ble Goude amekanusha mashtaka dhidi yake akisema hayatambui.
Gbagbo mwenye umri wa miaka 70 pamoja na waziri huyo wa zamani wa vijana ambaye anadaiwa kuwa mshirika wake wa karibu wote wanakabiliwa na mashitaka manne ya ukiukaji wa haki za binadamu yakiwemo ya mauaji na ubakaji yanayodaiwa kufanywa na wanajeshi watiifu kwa rais huyo wa zamani mwishoni mwa mwaka 2010 na mapema mwaka 2011 baada ya kushindwa katika uchaguzi uliomuweka madarakani Rais Alassane Ouattara.
Bensouda akanusha uvumi kuhusu mashahidi

Awali mwendesha mashitaka mkuu wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ya ICC Fatou Bensouda alisema lengo la kesi hiyo ni kuhakikisha kuwa inafichua ukweli kupitia njia za kisheria na kukanusha uvumi ulioonea kuwa kuna mashahidi wa uapande wa mashitaka katika kesi hiyo waliojitoa.

No comments: