KIMENUKA TENA HUKO INSTAGRAM: Zari na Wema Sepetu watukanana Instagram, soma walivyovuana nguo! - LEKULE

Breaking

19 Jan 2016

KIMENUKA TENA HUKO INSTAGRAM: Zari na Wema Sepetu watukanana Instagram, soma walivyovuana nguo!


Vita vikali vya maneno vimezuka Instagram kati ya Zari the Bosslady na Wema Sepetu. Vita hivyo vilianza baada ya kile kinachoonekana kuwa ni maneno kutoka kwa kambi ya Wema Sepetu kwenda kwa Mama Tiffah.

Zari aliamua kutoa ya moyoni kwa kuweka comment kwenye post yake mwenyewe baada ya matusi kutoka kwa kambi ya Wema kuzidi.

“Fake cars, fake houses, fake men, fake everything but they are here to judge.. yall look like just had a fight with a tiger,” aliandika Zari.

“We feel your pain Dee is a loving man. I know what you u missing but guess what, I gat it all by myself. Sent to hell on a one way ticket buried 6ft under #Kasepa #HeIsHappyNow,” aliongeza.

Wema aliamua kutokaa kimya, naye alijibu mapigo.

“Damn, she really got da energy,” aliandika.

“Mi siwezi jamani mambo haya. Kaka kajua kumchanganya dada. Sasa kama kachanganyikiwa si yeye. Mi ningejua kuwa kuna siku nitakuja kummiss kaka nisingemwacha. Akumbuke hilo kwanza. Halafu kingine, hivi mimi ni mwanamke pekee niliyewahi kuwa na kaka au?”

“Maana wenzangu naona hawatajwi ni Wemaa tu. Kuna kitu dada anakitafuta kwangu jamani. Sasa dada kama atasoma hapa ajue this is 2016, afanye mabadiliko basi maana tokea 2014 ana mimi tu, 2015 ana mimi tu na 2016 pia! Baby hujachoka tu bado? Nimejibu kwa mara ya kwanza maana naona umekuwa ukinitafuta muda mrefu mno. Mi maneno kama hayo yako sijui fake nini sinaga. But just if u read this honey, please nitoe kwenye ramani yenu. I no longer live there. And kuhusu kuwa fake, mi nishakubali na fake life yangu ila ningeomba utuwekee DNA ya Baby Tee kwanza. Pumbavu.”

Zari aliusoma ujumbe huo, akajibu:

“Ati DNA for what let her start na DNA ya Swiss then atupe ultrasound kisha ampime mtoto wake then she can ask for Tiffah’s. Hujawahi kuingia labour at unaomba DNA. Wachana na mambo ya wazazi. Endelea kugawa that’s the only thing you can manage. Mtoto wangu asikupe stress don’t beef with a baby, find you levels, Tiffah level nyingine# BabyBoss.”

Wema alituliza mizuka kwa kuandika post: Mama Taught me well…!! Kugombana na mtu mzima ni kukosa adabu…. Sijafunzwa hivyo…!”

No comments: