Jifunze Kutengeneza Pipi Za Kihindi ,uongeze Kipato Chako. - LEKULE

Breaking

21 Jan 2016

Jifunze Kutengeneza Pipi Za Kihindi ,uongeze Kipato Chako.



 ==>Wewe  ni  kijana  wa  kitanzania ?
 ==>Unataka  kuongeza  kipato  chako ?
Kama  jibu  lako  ni NDIO  basi   hii  ni  HABARI NJEMA  SANA  KWAKO. Taasisi  ya  NEEMA  INSTITUTE  OF  N.G.O  MANAGEMENT  kupitia MRADI  WA  UANZISHAJI, UENDESHAJI  NA USIMAMIZI  WA BIASHARA  NDOGONDOGO  inatangaza  nafasi  za  kushiriki  katika  SEMINA  YA  UJASIRIAMALI.   Somo  litakalo fundishwa  ni

 UTENGENEZAJI  WA  PIPI  ZA  KIHINDI.
Pipi  za  Kihindi  ni  bidhaa  inayo  pendwa  sana  na  watoto  wa  shule  ya  msingi  na  hata  sekondari.
 
Washiriki  katika  Semina  hii, watapewa nafasi  za  biashara  katika  shule mbalimbali  za  msingi  zilizopo  jijini  Dar  Es  Salaam.

ADA  YA  KUSHIRIKI  KATIKA  SEMINA  HII    NI  SHILINGI  ELFU   HAMSINI    TU (Tshs.50,000/=)

Fomu  za  kujiunga  katika  semina  hii, zinapatikana  ofisini  kwetu  kwa gharama  ya  Shilingi  ELFU  KUMI  NA  TANO  TU( Tshs.15,000/=).

Tunapatikana  UBUNGO   Dar  Es  Salaam, jirani  na  Shule  Ya  Msingi  Ubungo  National  Housing  nyuma  ya  jengo  la  Ubungo  Plaza.

Mwisho  wa  kuchukua  fomu  ni  tarehe  30  JANUARY 2016  saa  nane  kamili  mchana.

Semina   itafanyika  kwa  siku  tano,  kuanzia  tarehe  01  Februari 2016  hadi  tarehe  05  February 2016.

Kwa  maelezo  zaidi  kuhusu  semina  hii , wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  0766  53  83  84    AU   Tembelea  blogu  yetu :www.neemainstitute.blogspot.com

FAIDA   ZA  KUSHIRIKI  KWENYE  SEMINA  KUHUSU  MAFUNZO  YA  UTENGENEZAJI WA  PIPI  ZA  KIHINDI.
Taasisi   ya  Neema  Institute  Of  N.G.O  Management  yenye  ofisi  zake  jijini  Dar  Es  Salaam, katika  eneo  la  Ubungo  imeandaa    SEMINA  KUHUSU   UTENGENEZAJI  WA  PIPI   ZA  KIHINDI  ambayo  itafanyika  kwa  muda  wa  siku  tano, kuanzia  tarehe  01  FEBRUARY  2016  hadi  tarehe  05 FEBRUARI 2016.

Lengo  la  semina  hii  ni  kuwasaidia  wajasiriamali  wadogo  wadogo  na  wale  wa  kati, kupata  ujuzi  utakao  wasaidia  kuongeza  vipato  vyao.

Zifuatazo  ni   faida   za  kushiriki  katika  semina  hii:
1.Mafunzo  yanafundishwa  kwa  njia  ya  nadharia  na  vitendo  ( Theory  and  Practical )kila  siku  kwa  siku  zote  tano  za  mafunzo .  Katika  siku  zote  tano  utakazo  hudhuria  mafunzo  haya, utapata  kujifunza  kwa  vitendo  jinsi  ya  kutengeneza  pipi  za  kihindi. Lengo  letu  ni  kuhakikisha  kila  anaye shiriki  katika  semina  hii, anatoka  akiwa  amewiva  katika  suala  zima  la  utengenezaji  wa  pipi.

2.     NI    BIDHAA  YENYE  SOKO  LA  UHAKIKA :
Pipi   za  kihindi  ni  pipi  zinazo  tengenezwa  kwa  kutumia  malighafi  iitwayo   sukari  guru  pamoja  na   viambatano  (ingredients )  vingine .   Pipi  hizi  ni  bidhaa  inayo pendwa  sana  na  watoto  wanao  soma  katika  shule  za  msingi  na  sekondari .  Kwa  muda  mrefu sasa, wahindi  wanajulikana  dunia  nzima  kwa  kuwa   na  umahiri  mkubwa  wa  kutengeneza   vitu  vitamu  tamu pamoja  na  vyakula  vizuri  kwa  ujumla.  Hivyo  basi  suala  la  pipi  za  kihindi.

Utafiti  wetu  umetuwezesha  kugundua, kwa  biashara  ya  kuuza  pipi  za  kihindi   mashuleni, unaweza  kuingiza  faida  ya  kati  ya  shilingi  Elfu Thelathini  ( Tshs.30,000/=)  hadi   Shilingi  Elfu  Themanini  (Tshs.80,000/=)  kwa siku, kutegemeana  na  kiwango  cha  uzalishaji  wako.
 
 Na  kama  utapata  nafasi  katika  shule  zaidi  ya  moja, kipato  chako  kitakuwa  kikubwa  maradufu.

3.UHAKIKA  WA  KUPATA  NAFASI  YA  BIASHARA  KWENYE  SOKO  LA  UHAKIKA .
Baada  ya  kuhitimu  mafunzo,  kila  mshiriki, atapewa  nafasi  ya  biashara    katika  shule  ya  msingi  yenye  idadi  kubwa  ya  wanafunzi iliyopo  jijini  Dar  Es  Salaam  na  hivyo  kumuwezesha  kutengeneza  kipato  cha  uhakika, kupitia  biashara  ya  pipi za  kihindi. Sisi  kama  Taasisi  tunazo  nafasi  zaidi ya  mia ( 100 ) katika  shule  mbalimbali  za  msingi  zilizopo  jijini  Dar  Es  Salaam zenye  idadi  ya  wanafunzi  kati  ya  mia  nne  (400)  hadi  elfu  moja  (1000).
Nafasi  hizi  za  biashara  tutazitoa  kwa   watakao  hitimu  mafunzo  yetu.
 
Nafasi  hii  utaipata  baada  ya  kumaliza  mafunzo. Mafunzo  yanaanza  Jumatatu na  kuisha  Ijumaa. Siku  hiyo  hiyo  ya  Ijumaa  unapewa  details  za  shule  utakayo  enda  kufanyia  biashara  yako, Jumamosi  na  Jumapili, unazitumia  kufanya  maandalizi  ya  kutengeneza  pipi  zako, na  Jumatatu  unaanza  kuingiza  pesa  kupitia  shughuli  ya  kuuza  pipi  kwenye  shule  ambayo  tutakuwa  tumekupangia.

(  FURSA  YA  KUPATA  NAFASI  YA  BIASHARA  INAWAHUSU  WALIOPO  DAR  ES  SALAAM  TU  )

4.MTAJI  MDOGO  WA  BIASHARA :  Mradi  wa  kutengeneza  na  kuuza  pipi za kihindi  mashuleni, hauhitaji kiasi  kikubwa  cha  fedha  za  mtaji. Hata  kwa  wajasiriamali  ambao  ndio  kwanza  wanaanza  ujasiriamali na  hawana uwezo mkubwa wa  kifedha  wanaweza  kumudu.

5.UTAPATA  FURSA  YA  KUUNGANISHWA  NA  WAJASIRIAMALI  WENZAKO  NA  KUUNDA  TAASISI  ISIYO  KUWA  YA  KISERIKALI.

Washiriki  wa  mafunzo  haya, wataunganishwa  pamoja  na  kuunda  Taasisi  isiyo  kuwa  ya  kiserikali ( N.G.O ), ambapo  wata saidiwa  kuanzisha  VICOBA  pamoja  na  kufundishwa  utengenezaji  wa  bidhaa  nyinginezo  zinazo  pendwa  sana  na  watoto  mashuleni  kama  vile  Ubuyu  wa  Zanzibar  nakadhalika.

6.SEMINA  INATOLEWA  KWA  MUDA  AMBAO  HAUWEZI KUHARIBU  RATIBA  YAKO.
Kutakuwa  na  madarasa  ya  asubuhi  pamoja  na  madarasa  ya  jioni. Madarasa  ya  asubuhi  yanaanza  saa  nne  hadi  saa  sita. Na  madarasa  ya  jioni  yanaanza  saa  kumi  hadi  saa kumi  na  mbili  Hivyo  basi  kama  wewe  ni  muajiriwa  na   hauna  nafasi  muda  wa  asubuhi, unaweza  kupata  fursa  ya  kushiriki  katika  semina hii wakati  wa   jioni  kuanzia  saa  kumi  hadi  saa  kumi  na  mbili.

7.UNAWEZA KUJIFUNZA  KUTENGENEZA  PIPI  ZA  KIHINDI  NA  UKAAJIRI  VIJANA WENGI  WA  KAZI  NA  KUTENGENEZA  FEDHA  MARADUFU.

Unaweza  kujifunza  kutengeneza  pipi  hizi, halafu  ukatafuta  nafasi  ya  biashara  kwenye  shule  mbalimbali  za  msingi   na  kuwaweka  vijana  wa kazi.   Ukipata  nafasi  katika  shule  nyingi, maana  yake  hata  kipato  chako  kitaongezeka  mara  dufu.

Hizo  ni  baadhi  ya  faida  za  kushiriki  katika  mafunzo  haya.

KWA   WALIOPO   NJE   YA  MKOA  WA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam, mafunzo   haya yatatolewa  kwa  njia  ya  Posta. Utapatiwa  DVD  na  VITABU  vinavyo  elezea  STEP  by  STEP  kuhusu namna  ya  KUTENGENEZA  PIPI  ZA KIHINDI.

JINSI   YA  KUJIUNGA  NA  MAFUNZO  HAYA  KWA  WAOMBAJI  KUTOKA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kama  upo  nje  ya  mkoa  wa  Dar  Es  Salaam, na  unataka  kushiriki  katika  mafunzo  haya, tuandikie  barua  pepe  ya  maombi  ya  kushiriki  katika  mafunzo  haya. Barua  pepe  yetu  ni :  neemainstitute@gmail.com
 
Mwisho  wa  kupokea  maombi  ni  tarehe  30 JANUARY  2016.

EWE  MZAZI !  EWE  MLEZI ! UNA NGOJA  NINI ?
MLETE  KIJANA  WAKO  APATE   MAFUNZO  YATAKAYO  MSAIDIA   KUINGIZA  KIPATO  CHAKE.


EWE  KIJANA!  ZAMA  ZA  KUAJIRIWA  ZIMEPITWA  NA  WAKATI. USISUBIRI  KUAJIRIWA.  NJOO  UPATE  UJUZI  UTAKAO  KUSAIDIA  KUINGIZA  KIPATO KIZURI

No comments: