Hotel ya Mtoto wa Amani Karume yateketea kwa moto, Vijana wawili wahusishwa - LEKULE

Breaking

27 Jan 2016

Hotel ya Mtoto wa Amani Karume yateketea kwa moto, Vijana wawili wahusishwa


Moto mkubwa umeteketeza hoteli ya kitalii ya Konokono Beach Resort iliyoko Michamvi mkoa wa kusini Unguja, inayomilikiwa na mtoto wa rais wa zamani wa Zanzibar, Amina Karume pamoja na wawekezaji wawili kutoka nje ya nchi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kusini Unguja, Juma Saadi amesema kuwa moto huo uliteketeza nyumba tatu na mgahawa mmoja katika hoteli hiyo, ni watu wawili waliokuwa wakichoma nyasi karibu na hotel hiyo. Aliwataja vijana hao kuwa ni Meshak Amos Elisha na Mohamed Abdallah Hassan.

Kamanda Saadi aliwataka wananchi kupuuza habari zilizoenea zinazohusisha tukio hilo na mambo ya kisiasa, husasan vyombo vya habari vya kimataifa vilivyoripoti habari hiyo.

“Wakati wa kuchoma moto ndani ya uzio huo, ulizuka upepo mkali majira ya saa tano na nusu na kusababisha nyumba moja ya makuti katika hoteli ile kushika moto na kusababisha hasara hiyo,” kamanda Saadi alifafanua.


Kikosi cha zima moto na uokoaji kilifika katika eneo hilo na kufanya kazi za kuzima moto huo.

No comments: