Chuo kikuu cha Garissa chafunguliwa tena - LEKULE

Breaking

4 Jan 2016

Chuo kikuu cha Garissa chafunguliwa tena

Chuo Garissa
Kituo cha polisi kimejengwa ndani ya chuo
Chuo kikuu cha Garissa kilichofungwa mwaka uliopita baada ya watu 148 kuuawa kwenye shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa al-Shabab, kimefunguliwa tena.
Wafanyakazi wamefika kazini leo huku usalama ukiwa umeimarishwa.
Kila aliyekuwa akiingia katika chuo kikuu hicho kilichoko eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya amepekuliwa na maafisa wa usalama.
Kituo cha polisi, ambacho kitakuwa na maafisa zaidi ya 20 wa kutoa ulinzi, kimejengwa ndani ya chuo kikuu hicho.
Kitambulisha mada #GarissaUniversityReopens (Chuo Kikuu cha Garissa chafunguliwa tena) kimekuwa kikivuma katika mtandao wa Twitter nchini Kenya.
Wengi wanasema kufunguliwa kwa chuo hicho kunaonyesha Wakenya hawawezi kuvunjwa moyo na magaidi.
Msimamizi mkuu wa chuo kikuu hicho Prof Ahmed Warfa ameambia BBC kwamba wanafunzi wataanza kufika chuoni Jumatatu ijayo tarehe 11 Januari.
Hakukukuwa na sherehe yoyote maalum ya kuadhimisha kufunguliwa upya kwa chuo hicho.
  • Kenya yaomboleza shambulizi la Garissa
Wengi wa wanafunzi wanaofadhiliwa na serikali walionusurika shambulio hilo la mwezi Aprili walihamishiwa Chuo KIkuu cha Moi, Eldoret.
Wanafunzi wa kujitegemea ndio wanaotarajiwa kurejelea masomo Jumatatu.
Mwandishi wa BBC Bashkas Jugsodaay anasema kufunguliwa kwa chuo kukuu cha Garissa ni afueni kwa wakazi na viongozi wa mkoa wa Kaskazini Mashariki ambao wamekuwa wakiisihi serikali kufungua chuo hicho, kwa walikuwa wakikitegemea kwa ajira na wateja. Wengi walikuwa wakinufaika
Wanafunzi zaidi ya 800 walikuwa wakisomea taaluma mbalimbali katika chuo hicho kabla ya kushambuliwa na magaidi Aprili mwaka jana.

No comments: