Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Dodoma Bi. Ziada Nkinda (Aliyebeba Mtoto) akikabidhi zawadi za siku kuu ya Noeli (Christmas) zilizotolewa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa watoto wanaoishi kwenye kituo cha kuhudumia watoto cha kijiji cha matumaini Mkoani Dodoma.
Meneja
wa kituo cha kuhudumia watoto cha kijiji cha matumaini kilichopo Dodoma
Padiri Vicent, kwa niaba ya watoto wa kituo hiko, akimshukuru Bi.
ziada Nkinda kwa kukabidhi zawadi zilizotolewa na Mhe. Rais John Pombe
Magufuli zikijumuisha mchele kilo 121, Mbuzi wawili na mafuta ya kupikia
lita 40 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya laki sita.
(PICHA NA OFISI YA MKUU WA MKOA DODOMA)
No comments:
Post a Comment