JESHI
la Polisi Nchini limewatahadharisha madereva watakaozidisha idadi ya
abiria kuliko uwezo wa chombo cha usafari kwani ni kosa kisheria na
watakaozidisha abiria kwenye vyombo vyao vya usafiri watachukuliwa hatua
za kisheria.
Operesheni
hiyo inaanza leo baada ya tamko la Jeshi la Polisi na kuanza kutekeleza
kwa wale wote wataobeba abiria wengi tofauti na uwezo wa basi.
Watakaochukuliwa hatua ni madereva wa daladala,mabasi ya mikoani pamoja
na magari aina ya Noah.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la
Polisi, Advera Bulimba amesema kuwa Jeshi la polisi linaanza operesheni
ambayo ni endelevu na kuwataka watu wafuate sharia ya ubebaji wa abiria.
Advera
amesema kuwa katika kipindi hiki cha siku kuu Jeshi la polisi
limejipanga katika kuwadhibiti waendesha bodaboda kwa wataopandisha watu
zaidi ya wawili (mishikaki) kukiona cha mtema kuni kwa mujibu wa
sheria za usalama barabarani.
Aidha
amewataka wananchi kutoa taarifa za kihalifu katika msimu wa sikukuu
ili kuimarisha ulinzi wa watu na mali zao ili maisha yaweze kuendelea
baada ya sikukuu.
No comments:
Post a Comment