Taarifa ya Hali ya Mazingira Nchini inaonyehsa kwamba mwenendo wa uharibifu wa mazingira nchini ni wa kutisha. Mito mingi nchini inakauka.
Vyanzo
vingi vya maji vinakufa. Miti na misitu ya asili inapungua kwa kasi
kubwa – kila mwaka, tunapoteza zaidi ya ekari milioni moja za misitu.
Viwanda vingi havijaweka udhibiti wa kuzuia umwagaji wa kemikali zenye
sumu.
Uharibifu wa mazingira unaathiri sekta zote muhimu (kama vile kilimo, mifugo, uvuvi, utalii, uzalishaji umeme, makazi, miundombinu) na kupunguza uwezo wa nchi kupata maendeleo endelevu.
Uharibifu wa mazingira unaathiri sekta zote muhimu (kama vile kilimo, mifugo, uvuvi, utalii, uzalishaji umeme, makazi, miundombinu) na kupunguza uwezo wa nchi kupata maendeleo endelevu.
Tukiendelea
na mwenendo wa sasa wa uchafuzi wa mazingira, ndani ya kipindi kifupi,
mifugo na wanyamapori watakosa malisho (tumeshaanza kuona viboko
wanakufa kwenye Mto Ruaha kutokana na kukauka kwa mto), watu watakosa
maji ya kutumia, kilimo kitashindikana. Tunayo Sheria ya Mazingira ya
Mwaka 2004 ambayo inaweka makatazo mahsusi kwa nia ya kuepusha uharibifu
wa mazingira.
Serikali
ya Awamu ya Tano itahakikisha kwamba Sheria hii inatekelezwa kwa
ukamilifu wake. Pia, mapema mwakani, Serikali italeta mpango kabambe wa
kupambana na uharibifu wa mazingira, ambao utatoa wajibu kwa kila
mwananchi na kila taasisi ya umma na binafsi.
Kwasasa,
kwa kuanzia, tunaanza na operesheni ya kuwaondoa watu wanaoishi na
kufanya shughuli kwenye maeneo ya kingo za mito na maziwa, fukwe za
bahari, maeneo oevu (swampy) na maeneo ya wazi (Open spaces).
Kwa
hapa Dar es Salaam, zoezi la kuwaondoa wananchi waliojenga au kufanya
shughuli kwenye maeneo haya kinyume cha sheria na taratibu lilianza
rasmi tarehe 17/12/2015 likilenga kuwaondoa wananchi wote waliojenga na
wanaofanya shughuli kwenye maeneo hayo kinyume cha sheria.
Baraza
la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Wizara ya Ardhi
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kwa kushirikiana na mamlaka za Serikali
za Mitaa kwa pamoja wanaratibu na kusimamia zoezi hili linaloendelea.
Zoezi
hili limeanzia mtaa wa Mkwajuni, Kata ya Hananasifu Manispaa ya
Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Mpaka sasa zaidi ya nyumba 353
zimebomolewa katika mkondo wa Mto Ng’ombe unaomwaga maji yake Mto
Msimbazi. Wanaoishi au kufanya shughuli kwenye mabonde na kingo za mito
ya Mlalakuwa, Mbezi/Kawe na Nyakasangwe nao pia wanatakiwa kuhama.
Sheria zinazosimamia suala hili.
Zoezi
hili linasimamiwa na Sheria za Ardhi, Sheria za Mipango Miji na Sheria
ya Mazingira Sura ya 191 (Environmental Management Act Cap 191) ya mwaka
wa 2004 kwa Mujibu wa kifungu cha 55 inaelekeza kuwa maeneo ya kingo za
mito, miambao ya maziwa na bahari yanalindwa kisheria – na shughuli
zinazohusu ujenzi, kufukua, kuchoronga, kutoboa na kuharibu kingo au
mwambao ni kosa.
Kifungu
cha 57 cha Sheria ya Mazingira pia kinazuia shughuli zozote zinazoweza
kuhatarisha au kuathiri mazingira kutofanyika ndani ya mita 60 katika
kingo za mito, miambao ya ziwa na bahari ili kulinda maeneo hayo.
Athari za ujenzi kwenye Kingo za Mito
Kutokana
na ongezeko la watu jijini Dar es salaam, na maeneo mengine ya miji
yetu, uvamizi wa maeneo ya kingo za mito, mikondo ya bahari, maeneo oevu
umeongezeka.
Shughuli zinazofanyika kutokana na uvamizi huu ni pamoja na ujenzi wa nyumba, kilimo, ufugaji, utupiaji taka na uchimbaji mchanga.
Shughuli zinazofanyika kutokana na uvamizi huu ni pamoja na ujenzi wa nyumba, kilimo, ufugaji, utupiaji taka na uchimbaji mchanga.
Shughuli
hizi katika maeneo hayo husababisha uharibifu na madhara makubwa ya
mazingira hasa kipindi cha mvua ambapo maji hukosa uelekeo kutokana na
njia zake za asili kuzibwa na hivyo kutawanyika hovyo na kusababisha
mafuriko, uharibifu mkubwa wa miundombinu hasa madaraja ambayo
huvunjika, kukatika kwa barabara na vifo.
Athari zingine za kuvamia maeneo hayo ni kusambaa kwa magonjwa ya mlipuko yasiyoisha hasa kipindupindu kutokana na maeneo hayo ya mikondo ya mito kutokua na mfumo wa utoaji wa maji taka.
Athari zingine za kuvamia maeneo hayo ni kusambaa kwa magonjwa ya mlipuko yasiyoisha hasa kipindupindu kutokana na maeneo hayo ya mikondo ya mito kutokua na mfumo wa utoaji wa maji taka.
Serikali
ya Awamu ya Tano haitakubali kuacha hali hii iendelee. Tumeamua, kwa
kushirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ardhi na Mamlaka za Serikali za
Mitaa kote nchini, kuchukua hatua kurekebisha hali hii.
Kama
alivyosema Waziri wa Ardhi, kwasasa, zoezi hili litasimama kwa muda
kutoa nafasi ya mwisho kwa wale wanaofanya shughuli na kuishi katika
maeneo haya kuondoka kwa hiari yao kwa kuwa taarifa na notisi rasmi
walikwishazipata mara nyingi siku za nyuma. Baada ya mwaka mpya zoezi
hili litaendelea.
Vilevile,
kwa taarifa hii, naelekeza na kukumbusha kwamba zoezi hili litaendelea
nchi nzima. Kwa maana hiyo, yoyote yule aliyejenga na anayefanya
shughuli zinazoharibu mazingira kwenye kingo za mito, vyanzo vya maji,
miambao ya maziwa na fukwe za bahari kinyume cha sheria, ajiondoe mara
moja kwakuwa kuanzia mwakani tutatimiza matakwa ya Sheria bila kusita.
Kuwa na vibali vingine vya ujenzi au shughuli katika maeneo haya, hakuondoi uwezo wa kutekelezwa kwa Sheria ya Mazingira.
Kuwa na vibali vingine vya ujenzi au shughuli katika maeneo haya, hakuondoi uwezo wa kutekelezwa kwa Sheria ya Mazingira.
January Makamba (MB)
Waziri wa Nchi, OMR – Muungano na Mazingira
22.12.2015
No comments:
Post a Comment