COSOTA yataja kiasi atakacholipwa msanii kwa kila wimbo au video itakayochezwa kwenye Redio au TV - LEKULE

Breaking

23 Dec 2015

COSOTA yataja kiasi atakacholipwa msanii kwa kila wimbo au video itakayochezwa kwenye Redio au TV


Miongoni mwa maswali mengi ambayo yanaendelea kuulizwa kuhusiana na utaratibu mpya wa vyombo vya habari kuanza kuwalipa wasanii kwa kucheza nyimbo zao kuanzia mwakani, ni pamoja na kiasi gani msanii atakuwa analipwa.
 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Hakimiliki Tanzania (Cosota), Doreen Sinare alisema kuwa wanamuziki, watunzi na maproducer watalipwa asilimia 60 kwa kila wimbo au video itakayochezwa katika redio na televisheni yoyote ndani na nje ya nchi kwa kutumia vifaa bora vilivyowekwa na kampuni ya CMEA.
 
Doreen alisema kuwa mwanamuziki, msanii alitakiwa kupata asilimia 70 ya kazi yake, lakini asimilia 10 itakatwa katika malipo hayo na kuingia katika mifuko ya jamii kwa mahitaji yake ya baadaye.
 
Alisema kuwa wanamuziki ni sawa na wafanyakazi wengine na asilimia 10 hiyo itamwezesha kujipatia kipato chake kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine katika taasisi mbalimbali.
 

COSOTA kwa kushirikiana na kampuni ya kusimamia kazi za wanamuziki nchini Copyrights Management East Africa Limited (CMEA) wataanza kulipa mirabaha ya wanamuziki na wadau wake kuanzia mwakani.

No comments: