Davido atoa uthibitisho mwingine kuwa hakuna ‘beef’ kati yake na Diamond - LEKULE

Breaking

2 Jul 2015

Davido atoa uthibitisho mwingine kuwa hakuna ‘beef’ kati yake na Diamond

Bado una wasiwasi juu ya maelewano kati ya muimbaji wa Nigeria, Davido na Diamond? Pamoja na Diamond kujibu kwenye Interview mbalimbali kuwa hawana tatizo, Davido naye ametoa uthibitisho mwingine kuwa hakuna ‘beef’ kati yao.

Ni jambo gumu kupost kitu kinachomhusu mtu ambaye hamna maelewano, ndio maana kwa post hii ya Davido watu wanapaswa kufahamu kuwa jamaa hawa wawili wanaiva chungu kimoja, na tutarajie kuwaona wakitumbuiza tena pamoja kwenye tuzo za MTV mwezi huu.
 

Baada ya MTV kutaja majina ya wasanii wa Afrika watakaotumbuiza wakati wa utolewaji wa tuzo za MAMA akiwemo Davido na Diamond, Davido alipost picha ya performance aliyofanya na Diamond mwaka jana kwenye tuzo hizo.

No comments: