Afande Sele amesema akiingia bungeni hawezi kuwasahau wasanii wenzake
kama walivyosahauliwa na wasanii wabunge waliotangulia kuingia
mjengoni.
Rapper huyo atawania kiti cha ubunge wa jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi
cha ya chama cha ACT na amesemakuwa akiingia bungeni wasanii
watarajie mambo makubwa kutoka kwake.
“Lengo langu kubwa kwa wasanii ni kupigania haki za wasanii,” Amesema Afande Sele
“Nimegundua tukizungumzia haki za wasanii kwenye muziki kwa kuimba
tu, hakuna kitachofanyika. Viongozi hawana shinikizo la kutekeleza,
wanazungumzia tu kidogo halafu wanaacha.
"Lakini nimeona ukiingia bungeni
wasanii tutashiriki moja kwa moja kwenye utungaji sheria za nchi.
"Suala
la haki za wasanii nitakuwa niko nalo karibu sana na nitalipigania kwa
namna yoyote kwa sababu nipo kwenye chombo cha maamuzi na nina rungu
mkononi,” ameongeza msanii huyo.
“Lakini leo hii hata nikiwa nazungumza sina silaha yoyote, lakini
tukiingia bungeni tunaweza kupaza sauti na zikasikika kwa sababu tupo
kwenye chombo cha sheria na kina mamlaka na uwezo.
"Unajua kila
anayeingia bungeni unakuta baadaye anabadilika, mimi nina upeo mkubwa
tofauti na wabunge wanaomaliza muda wao. Inaonyesha waliingia kwenye
siasa kwaajili ya kutafuta maslahi. Kwahiyo wasanii watarajie kuona
sheria za haki miliki zikipatikana au zile zilizopo zikifanyiwa
marekebisho,” amesisitiza.
“Kwa sasa hivi bungeni hakuna mtu mwenye uchungu na sanaa, wasanii
ambao walibahatika kuwa wabunge wameingia bungeni nao wamegeuka mafisadi
vilevile.
"Wamekuwa wawekezaji wa biashara, wamedharau shida za wasanii.
KwaHiyo mimi nafikiri bungeni kulikuwa hakuna wasanii ambao
wanatuwakilisha, wasanii tunaotaka kuingia bungeni sasa hivi tuna wito.
Kwahiyo watu wategemee kuona mabadiliko makubwa sana kwenye sanaa.”
Katika hatua nyingine, Afande amesema kwa sasa hatoweza kutoa wimbo wowote mpaka uchaguzi utakapopita.
“Ningependa sana mashabiki wa muziki wangu wasubiri uchaguzi upite
ndio wasikie kazi mpya kwa sababu tayari akili na mawazo na malengo
yangu yapo kwenye uchaguzi. Mimi nimeona nisiwa-disturb kwa kitu
chochote mpaka uchaguzi upite.
"Kwa sababu hili ni jambo muhimu sana linatokea kwenye taifa na ni maisha yao. Kwahiyo watu wajitokeze kujiandikisha pamoja na kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka.”
"Kwa sababu hili ni jambo muhimu sana linatokea kwenye taifa na ni maisha yao. Kwahiyo watu wajitokeze kujiandikisha pamoja na kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka.”
No comments:
Post a Comment